- Mbunge wa eneo bunge la Baringo Kusini, Grace Kipchoim alifariki siku ya Ijumaa, Aprili 20
- Ujumbe wake wa Facebook uliashiria kuwa alitarajia lolote tu na hivyo akazidi kuwatia moyo wafuasi wake
Mbunge wa Baringo Kusini, Grace Kipchoim aliaga dunia siku ya Ijumaa, Aprili 20 akiwa katika hospitali ya Nairobi Hospital alipokuwa akipokea matibabu baada ya kuandamwa na saratani ya tumbo kwa muda mrefu.
Habari Nyingine: Video ya Otile Brown akimpapasa Vera Sidika matiti yadhihirisha kuwa walilala pamoja
Sasa imebainika kuwa Grace alikuwa ameshajiaandaa kwa ajili ya kifo chake kupitia kwa ujumbe aliouchapisha katika ukurasa wake wa Facebook.

Habari Nyingine: Rais Uhuru hatimaye azungumza kuhusu makubaliano yake na Raila
Siku kumi kabla ya kifo chake, mbunge huyo alikuwa akiwatia moyo wafuasi wake kuwa yupo, jambo lililoonekana kama kuwapa kwaheri.
Aliwaomba wafuasi wake kutokufa moyo maishani na kufanya mema maishani bila kujali maneno ya watu.
Tuma neno ‘NEWS’ kwa 40227 ili kupata habari muhimu pindi zinapochipuka
Habari Nyingine: Binti alalamika baada ya kufukuzwa kanisani kwa "kuvaa vibaya" (picha)
“Kuwa mtu mwema ni kama kuwa mlinda lango. Hata ukizuia magoli mangapi, watakulaumu kwa moja ulilofungwa. Usife moyo kwa yale watu watasema kukuhusu…Tenda Wema, Nenda Zako!,” Alimalizia katika ukurasa wake wa Facebook, siku kumi kabla ya kifo chake.
Kama ilivyoripotiwa na TUKO.co.ke, Grace alichaguliwa tena kwa awamu ya pili kwa tiketi ya chama cha Jubilee.
Read ENGLISH VERSION
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri: mwangi.muraguri@tuko.co.ke
Subscribe to watch new videosChanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdibH53hJdmpJqmlaO8bq3LorCosZGvwq%2Bz1KaxmmWdrLa0tM5mpJutnpyybsPAZpmaqpmjtLB5yq6qoqaZYri2wMCboKuhXaC2p7uMnJ%2Bao5VjtbW5yw%3D%3D